Sunday, August 1, 2010

UTABIRI WAKE UMETIMIA?

Dada Digna

Alikuja ghafla katika tasnia ya blog kisha akatoweka ghafla, lakini nimefanya upekuzi wangu nimepata taarifa kuwa alikuwa akilea ujauzito na amejifungua binti na amempa jina la Larissa.

Nimemkumbuka dada huyu Digna Abraham kutokana na utabiri wake kutimia, Je ni utabiri gani huo? Usipate tabu msomaji unaweza kubofya hapa kumsoma.

Hongera dada kwa kutuletea kabinti kazuri, tunamuomba mungu akakuze kwa umri na kimo ili nako kaje kawe mwanablog mahiri kama mama yake. Hongera Digna

6 comments:

Maisara Wastara said...

Dada mdogo Koero, ni kweli utabiri wake umetimia...
Ningependa pia kuchukua nafasi hii kumpa pongezi kwa kupata mtoto.
nakukaribisha kwenye ulimwengu wa kina mama.
Tupo pamoja dada Digna, tunakumba urejee kwenye ulimwengu wa blog tusome fikra zako pevu

Yasinta Ngonyani said...

Nami sipo nyuma , ni kweli Da Digna aliåpotea ghafla nakusifu Koero kwa upekuzi wako. Digna karibu sana kwenye ulimwengu wa malezi. Hongera sana kwa kupata mtoto na pia kwa kuwa wazazi/walezi. Nakutakieni maöezi mema.

Anonymous said...

Kumbe wajanja wamekudengua. Duh! Sasa kuwa mjamzito ndiyo unaacha kublogu au jamaa ni mkoloni! Congratulations ANYWAY...

kamala Lutatinisibwa Lutabasibwa said...

safi sana, mwombeki kapata mwenza sasa

chib said...

Anony... Duh!

DLOMEN said...

:)