Friday, September 18, 2009

SALAAM ZA MAKABILA YETU

Kijijini kwetu

Wasomaji wapendwa wa blog hii isiyoisha vituko, Kwa sasa niko jijini Dar es salaam nimerejea kimya kimya na leo nilikuwa najaribu kufanya utafiti wa lugha za makabila yetu hapa nchini. Kwa mujibu wa tafiti inasemekana kuna makabila zaidi ya 120 hapa nchini.Niliamua kuangalia zaidi salaam, hususan za asubuhi, Kutokana na utafiti wangu nimepitia makabila kadhaa na kukutana na maneno yanayotumiaka katika salaam za asubuhi ambayo yanafanana kidogo, hebu tuone maneno hayo ni yapi:


KINGONI: Uyimwiki = Habari za asubuhi

KIZIGUA: Kugona vihi = Habari za asubuhi

KINYAKYUSA: Ughonile = Habari za asubuhi

KIYAO: kwimukaga = Habari za asubuhi

KIPARE: Murevuka = Habari za asubuhi

KIUNGUJA: wambaje = Habari za asubuhi

KISAMBAA: Onga makeo = Habari za asubuhi

KIANGAZA: Mwalamtse = Habari za asubuhi

KINYAMWEZI: Mwangaluka = Habari za asubuhi

KICHAGA: Shimbonyi = Habari za asubuhi

KIMERU: Konumbware = Habari za asubuhi

KIMASAI: Sopai = Habari za asubuhi

KISUKUMA: Mwadila = Habari za asubuhi

KIHEHE: Kamwene = Habari za asubuhi

KIBENA: Kamwene = Habari za asubuhi

KIKINGA: Ulamwihe = Habari za asubuhi

KINYIRAMBA: Ulalaliani = Habari za asubuhi

KIHAYA: Wabonaki = Habari za asubuhi


Kwa leo naishia hapa mwenye nyongeza anaweza kuongeza ili tujifunze pamoja.
Tukutane wakati ujao

23 comments:

  1. Asante sana dada Koero kwa kutupa hizo,salam nyingine hata nilikuwa sizifahamu,mmmh ila hiyo ya kisukuma hebu fanya utafiti kidogo.

    ReplyDelete
    Replies
    1. Yes amekosea sio mwadila ni Mwangaluka ndo mana ya habari za asubuhi hiyo mwadila inatumika mchana na jioni mpka usiku

      Delete
  2. wewew kihaya umechamsha. Wabonaki sio za asubuhi bali ni mambo vp

    ReplyDelete
  3. Jamani kukosea ndio kujifunza.
    kamala, mambo vipi, yawezekana ikawa ya asubuhi au ya jioni...au?
    na dada Schola hilo la wasukuma niliambiwa tu si unajua kuuliza si ujinga...au nimedanganywa mwayego.....LOL
    haya na wengine wekeni changamoto zenu humo.....

    ReplyDelete
  4. Koero nawe asante sana kwa salamu hizi. Hapo kwenye kingoni unaweza kusema UYIMWIKI kama ulivyosema au pia HABARI ZA LUKELA ni sawa tu. Nimefurahi kweli haya uyimwike. KIMATENGO: Kujumuka= Habari za asubuhi

    ReplyDelete
  5. Sasa mie napenda salamu hizi zikitafsiriwa moja kwa moja. Mfano WABONAKI itafsiriwe kama "umeona nini?"
    Hahahahaaaaaaaaaaaaaa. Niliku-miss dadangu. Nasubiri "vijimambo" vya huko ulikopotelea.

    ReplyDelete
  6. Nakupa big up kwa kutuletea salamu kadha wa kadha.
    Naomba kufanya marekebisho kidogo kwenye Kibena, nadhani na Kihehe yanaweza kuingiliana.
    Katika Kibena, Kamwene ni salamu unapokutana na mtu kwa mara ya kwanza pasi kujali ni asubuhi, mchana ama jioni.
    Salamu itumikayo kumaanisha 'habari ya asubuhi' husemwa 'ulamwihe' ama 'ulamwihe wuli' ambayo kwa tafsiri ya moja kwa moja ya kimsamiati ni kusema 'umeamkaje'
    Sina hakika na Kihehe, sina ujuzi nacho. Lakini nina hakika na Kisangu cha huko Mbarali, Mbeya kwani kinaingiliana sana na Kibena.
    Ahsante sana da Koero. Wikendi njema.

    ReplyDelete
    Replies
    1. Na mie naomba nikurekebishe kwenye kibena, kamwene hutumika kwa watu wasioonana mda mrefu, kama mnaonana kila siku wanatumia "ulamwike" mkinga "ulamwihe" mpangwa "ulamwikhe" tofaut ya makabila haya matatu ni matamshi na rafudhi tu.

      Delete
  7. Hili ni somo la bure, siku nyingine utuwekee na jinsi ya kushukuru

    ReplyDelete
  8. koero

    wabonaki ni kwa mkubwa kwenda kwa mdogo. vinginevyo inabidi ilembwe lembwe.

    za asubui ni OloileOtai au plural Mulailemtai

    ReplyDelete
  9. waongelamo?-kijita. na pia Wachio nade?-kijaluo

    ReplyDelete
  10. Kinyaki pia hutumia 'ukwasilee' (akiwa mmoja) na 'mkwasilele' (wakiwa wengi), lakini mara moja moja sana.

    Mzee wa changamoto: salamu nyingi za kibantu hazitafsiriki vema ikiwa unataka iwe hivyo. Pengine mwanzo ilikuwa hivyo lakini hali ya kutumika kama salamu inazififisha maana za kimaneno moja moja.

    mfano 'shikamoo' na mdogo wake 'marahaba' tukizifuata maana zao tutakuwa hatusalimiani, uwongo?

    salamu kama 'habari za asubuhi/mchana na kadhalika' huwa haina maana hasa kujua 'hali' husika. ndio maana majibu ya salamu hii asilmia kubwa (pengine 96+) ni 'nzuri'. maana ya salamu hizi ni kutambua na kutambulika katika jamii na uwapo wa wanajamii wenyewe. ingawaje hata hivyo maana za naneno yaliyomo katika salamu zetu hayafishwi katika matumizi yasiyo salamu.

    ReplyDelete
  11. Mwangaluka kisukuma za asubuhi. Mwadila ni jioni... tambua ya kuwa kinyamwezi na kisukuma salamu hazitofautiani

    ReplyDelete
  12. Kisukuma umechemka mzeiya, mwadela sio habari za asubuhi, mwadela ni habari za mchana/jioni/za kushinda

    ReplyDelete
  13. KUSUKUMA - Mwangaluka - habari za asubuhi.

    ReplyDelete
  14. Hapo kwenye kinyakyusa Habari ya asubuhi tunasema "otwa lobhonjo" au "mlembwike" au neno mghonile hutumika wakati wowote iwe asubh mchana au jioni japo hata mchana tunasema mwangele au otwo pamuse na usiku tunasema otwa pakeloo" ambapo huweza kujibizana "mghonile" "mghonile" "ndaga" "ndaga"

    ReplyDelete
  15. Wangaluka.. Walampola... Kinyamwezi..

    ReplyDelete
  16. Je habari za asubuhi tunasemaje kwa kwa lugha ya
    kibondei?

    ReplyDelete
  17. Mtu akikwambia usindile unamjibu vp

    ReplyDelete
  18. Wajibu namna hii mpola za kukaya. Au eit ale mpola du

    ReplyDelete
  19. Mbona sisi waha umetusahau?

    ReplyDelete

Andika maoni yako, Tujadili kwa kina