Monday, August 29, 2011

HATIMAYE MTUHUMIWA AJISALIMISHA!!!!



Haya jamani kilio cheni nimekisikia, jana ndio nimefika Dar nikitokea Tanga, Nilikuwa Tanga, kwa dada yangu ambaye alifanikiwa kuongeza idadi ya watu hapa duniani mwezi uliopita. kwa kuwa hakuwa na mtu wa kumsaidia, nililazimika kwenda kule kumpikia uji na mtori.

Nimerudi na tupo pamoja.


13 comments:

Yasinta Ngonyani said...

Ulifanya vizuri kwenda kumsaidia dada lakini ulichokosea kutokuaga...lakini sawa sasa upo nasi tena ni furaha kwa kweli KARIBU SANA:-)

PASSION4FASHION.TZ said...

KARIBU SANA,UNGEAGA DADA WATU WASINGEENDA KUCHUKUA RB....LOL, VIPI HALI YA MAMA NA MTOTO?

Koero Mkundi said...

Samahani jamani, mie nilijua naenda kumsalimia tu na kumpongeza, lakini nilipofika nikakuata mfanyakazi wake wa ndani kasepa kwa madai kuwa hawezi mambo ya kulea watoto. bibie nikajikuta nikishika jukumu hilo.

Kwa kweli kazi ya kutafuta mtumishi wa nyumbani ni ngumu kweli siku hizi tofauti na zamani, sijui ni hizi shule za kata.....LOL.

Tumehangaika sana kutafuta mtumishi wa ndani kwa takriban mwenzi na ushee, hatimaye akapatikana, ikabidi nikae kidogo ili kumfundisha na kufanya hand over, na ndipo nikaondoka kwenda Arusha nikakaa kule kwa wiki moja na jana ndio nhiakrudi DAR.

Kwa kweli niliwa-miss sana ndugu zangu..

o'Wambura Ng'wanambiti! said...

karibu tena mamito!

Simon Kitururu said...

Karibu tena mwanakwetu!

Lakini lini wewe utasaidia kuongezea idadi ya watu Dunia ,..
....ili Dunia iwe na akina Koero wengi?

kamala Lutatinisibwa Lutabasibwa said...

hii inamaanisha miezi kadhaa iliyopitadadako ilifanya siri iliyogeuka kuwa hadharani mwezi ulopita, siri si siri tena! nawewe umo safarini, si unapenda mambo ya sirini?

Fadhy Mtanga said...

...sasa wakati ushafika Koero binti Mkundi mimi nawe tushirikiane kuongeza idadi ya watu hapa duniani. Madhali usharudi Dar tufanye hima kabla mtani wangu Markus hajaleta songombingo zake na kijinopembe!

emu-three said...

Ndugu yangu watu tunatafuta kazi wewe wasema utafuta watu wa kazi! LAKINI kweli kumpata mtumishi wa ndani ni kazi kweli kweli , maana wapo , lakini kuna kitu `tabia'....
Karibu tena ...TUPO PAMOJA

MARKUS MPANGALA said...

MTANI WANFU FADHY. nimekupa huyu binti umnong'oneze tu ila sikati kujua unachomnong'oneza. ole wako ulete vurumai, nitamwondoa tena na hiyo itakuwa kifisadi kweli kweli ha ha ha ha ha ha ha kumbe unaniogopa eeeeehhh umeona eeeh hadi unasema nilimtorosha ha ha ha ha acha watu tule rahaaaa bwana mzee Mkundi mtu poa ana bidi maridadi kweli kweli. yaani ukipta mtaani ukimtambulisha jamaniiiii huyu ndiyo mama mwenye nyumba yanguuuuu hivyo tunatarajia kuleta mitoto mitano iliyoshba. Lol sipati picha hao watoto wete honey wangu Koero ha ha ha sema Haniiiiii

Fadhy Mtanga said...

mtani mie wala sitishiki ng'oo

Obat Kuat Asli said...

I like it this blog information, thanks for sharing

Vimax Asli Canada said...

I like it this blog information, thanks for sharing

poker said...

PROMO DELIMA
poker online | Agen Domino | Agen Poker|Kumpulan Poker | bandar poker | Judi Poker | bandar qiu | Judi online terpercaya

Bonus yang kami sediakan :
* TO (Turn over) sebesar 0.3% yang akan di kami bagikan setiap hari senin
* Bonus referal sebesar 10%

Ayo segera daftarkan diri anda dan bergabunglah bersama kami !!
Delimapoker.com Situs Agen Poker Online Terpercaya di Indonesia akan melayani Anda dengan profesional, memproses depo/wd dgn cepat.
Come join and be a winer with us !!

Untuk info selanjutnya silakan chat ke :
Livechat_____: delimapoker
BBM__________: 7B960959
Facebook_____: Facebook
Phone number_: +85595678845
pendaftaran___http://www.delimapoker.com/?ref=19860605