Friday, September 2, 2011

WANAUME BWANA, HIVI MKIONA UCHI WA MWANAMKE MNAPATA NINI?

Wanaume wengine hata wakiona hivi huchanganyikiwa!



Kuna wakati huko Berlin, nchini Ujerumani, kulikuwa na unesho ambapo wanawake walikuwa wakionesha maungo yao kwa malipo. Wanawake hao walikuwa wakionesha maungo hayo kwa wanaume ambao wanaamini kwamba, kuona sehemu uchi wa mwanamke ndicho kilichowaleta hapa duniani.


Hebu sikia ujinga huo zaidi. Waandaaji wa onesho hilo ambalo lilihusisha wanawake wapatao 100 wa umri wa miaka 19 hadi 65 walilazimika kuwaita Polisi ili kudhibiti midume iliyokuwa ikifanya fujo wakati wa kukata tiketi kila mmoja akitaka awe wa kwanza kuingia kwenye onesho hilo.


Kila mmoja alikuwa akitaka awahi yeye kuona sehemu za siri ambazo bila shaka mkewe na watu wengine wa jinsia ya kike wanaomzunguka wanazo!


Mwandaaji wa onesho hilo, Vanessa Beecroft, ambaye ndiye mgunduzi wa njia hii ya kujipatia fedha kirahisi kutoka kwa wanaume hao wasio na haya, hufanya maonesho haya kwa jina la VB55 kwa nyakati na miji tofauti Ulaya.


Msije mkashangaa siku akija na huku Afrika kujichotea mamilioni ya dola, au akajitokeza mjanja mwingine huku Afrika na kuanzisha hayo maonesho, naamini wanaume watauana wallahi.

22 comments:

Yasinta Ngonyani said...

Koero, Si utana wanaume watauana kwa kweli....Kaazi kwelikweli!!

sam said...

unajuwa ,sisi wanaume, mbeleya wanawake jeuri hakuna.ni wababe kwanje,lakini kwandani niwadhaifu sana.kwahiyo kitu chochote kinacho onyesha umbile la mwanamke,awe uchi,kavaa,ilimradi kuna kadalili ka mvuto mwanaume lazima atetereke kidogo.Nahii hasa kwa wadada wa kiafrika,wa kizungu siyo sana.lakini si utani inataka moyo kushuhudia wanawake 100 wako uchi,mimi siwezi wala hilo onesho nalinipite. dada koero je ikiwa niwanaume wako uchi kwa idaddi hiyohiyo,100,katika onesho wanawake hawatauwana??
kaka S.

Simon Kitururu said...

Ila tamaduni inachangia. Nchi kama FINLAND na tamaduni zao za SAUNA kumuona mwanamke yuko uchi hata ikiwa ni mama yake wala hatishiki mtu! Na kitu kimoja ukifika katika nchi kama FINLAND utastukia hata matangazo ya TV kuwa na binti au KIDUME uchi wala sio kitu cha ajabu!


Na hukawii kukuta wadada na wanaume wako uchi sauna kikawaida tu na hadindi mtu!

Tatizo ni sie ambao tumekuzwa kwa kufichwa sehemu za siri!

sam said...

Mtakatifu,kuficha /kufichwa uchi kwa siri nitatizo!!?nafikiri waliwaza mbali sana wazee wetu waliotukuza kwa kufichwa uchi,kuna raha yake.na kama ulivyo sema kila mtu na utamaduniwake.huku kwangu,uk, mtangazaji mmoja elmaarufu ,wa TV moja alituonyesha,matako kwa kuina katikati ya kipindi,lakini haimananishi hakuna waliotamani takolake!

haya wahenga walisema MFICHA UCHI HAZAI.kaka S.

Simon Kitururu said...

@Kaka S:Nafikiri nilitumia neno tatizo vibaya!

Kwa kuwa nakubaliana sana na malezi yetu kuliko ya Kiscandinavia katika hili . Na kutokana na makuzi yangu huwa naona burudani sana nikishuhudia mtu kwa maraya kwanza akidondosha nguo mbele zangu -yani kitendo kizima hicho cha upanguaji wa nguo kama tu starehe ya kutongozana kabla sijakubaliwa huwa naona zina ladha yake mwanana sana labda ndio maana nisinge penda kuunganishiwa kimwana kama wafanyiwavyo baadhi na wazazi !

Anonymous said...

HUO NDIO UUME KAMA SIO UANAUME! UCHI wa MWANAMKE ni CHAKULA KIKUU cha DUME iwe ni kuona tu au hata kuonja!! Kinyume chake utakuwa unampinga MUUMBA aliyeumba uume na uke!!!!
Wanawake nao wanatamani. Wakikosa MUHOGO halisi wananunua TOYS za kucheza nazo!!!!!

Unknown said...

Kabla ya wakoloni hivi tulikuwaga tunaishije kwa kuvaa vile.

Goodman Manyanya Phiri said...

@Mcharia

Kwani mavazi yale yanatatizo gani? Kwani historia ya binadamu hujui kwamba Mswahili ndie mwanzilishi kwanza wa familia na hapo baadaye uficha-uchi (REPRODUCTIVE ORGANS) wakati mkoloni unayetaka kumnyanyuwa alikuwa bado anatembea uchi kabisa na kukaa kwenye mapango huko Ulaya?


Ningependekeza uvitembelee kidogo kwanza vitabu vyake Msomi Mazrui wa huko Kenya ili kuelewa kwanini ziwa kwa Waswahili wengi ni chakula cha mtoto tu katika familia wakati kwa wengine hilohilo ziwa la mwanamke ni chakula cha uume!

Anonymous said...

asante kwakuweka kitu roho inapenda maana hapo mwanaume razima uchangamke halafu mimi nimemchagua wakushoto ona kilekinguo kilivyo kaasehemu safi leo usingizi utakuwa mzuri tu.hivi nanyinyi wanawake mnapenda kuwaona wanaume wakiwa uchi?

o'Wambura Ng'wanambiti! said...

duh!

MARKUS MPANGALA said...

mmmmmmmmmH!

chib said...

Mambo ya kuwajumuisha watu wote kama ati samaki mmoja akioza..., khaaa!
Kuna wanaume wengine wakiaga nyumbani wanaenda kazini, basi ujue kazi yao ni kukagua hizo mnazozosema zinaleta tamaa za fisi. Na wanaona hivi vitu ni vya kawaida sana na wala haviwapi msisimko wowote. Kama unabisha, nenda pale wadi ya wazazi au ya akina mama.
Lakini.... na hao wakina dada wanaokubali kuachia wazi ili wapate kipato, hatupaswi kuwanyooshea kidole au....

Mbele said...

Dada Koero, ya leo kali. Haya maonesho yakitinga Bongo, njemba tutapiga foleni kuanzia asubuhi, na foleni yenyewe itabidi mgambo wenye bunduki kuidumisha kwa usalama. Patakuwa hapatoshi :-)

Anonymous said...

sasa huu ni ujinga gan? ina maana hawa wanawake wa kiafrika walikua wakionyesha maungo yao mbele ya wazungu huko Berlin? ama! mbona wazungu siwaoni hapo??

Anonymous said...


Mbele ya K, mtatulaumu sana!

Anonymous said...

Nina utaalamu wa Saikolojia ya Binadamu. WANAWAKE msishangae. Ni Vile Mungu alimuumba Jinsia ya Kiume ya Kiumbe chochote kilicho hai kiwe na matamanio kwa kiumbe chenzake cha Jinsia ya Kike. Kwa ajili ya Kusababisha lile tendo ambalo kwalo wewe leo upo dunia hii ya viumbe hai ama wa Wakike/Wakiume.Pia alimpa Kiumbe wa Kiume kazi kubwa ya kushawishi mwenzake wa Kike kuelekea tendo hilo. Unaweza kuona mifano katika kuku, mbwa, ng'ombe,mbuzi n.k n.k akiwemo binadamu mwenyewe ila kila kimoja kwa style yake na katika mazingira yake muafaka.

Nahisia za kiumbe wa kiume ziko machoni pake na ni za haraka kiasi ukilinganisha na za kiumbe wa kike. Yote Mungu ndie aliye taka hivyo kwanini? Anajua yeye! Kumbuka Mungu ndiye Mwanasayansi Mkuu kuliko wote uliopata kuwasikia dunia hii. Sababu hao wana Sayansi wanafatafuta kwanini from God's Creation. Ila Mungu already ana majibu. Na akipenda anawafunulia wanaelewa au mengine yanbaki hayana majibu kama haya.

Ukweli ni kwamba saikolojia ya M.ume ni tofauti kabisa na ya Kike na KAMWE haziwezi kuwa sawa.

LAZIMA atatamani kwa kuona, nahii inamsaidia kupeleka taarifa kwenye Ubongo na kutafsiri kuwa panakitu cha namna hii na ni Kitamu/Kibaya inategemea na sifa zingine ambazo moyo wake unazitaka na hv Ubongo ukitafsiri POSITIVELY inapelekea UUME kusimama tayari kwa lolote au basi tu kuridhisha nafsi ikitegemea pia na mhusika (m.ume sasa)kwa kiasi gani anaendelea kuirusu taarifa hii kusafiri. Ndio maana katika HALI YA KAWAIDA huwezi kukuta taarifa ikaruhusiwa kusafiri kama jinsia hii ya kike ni Mama, Dada au kwa yeyote mwenye mahusiano ya Damu. Moyo/Roho inakataa!

Kwa hivi wanawake furahieni jambo hili manake kama M.ume asipokutamani kwa kukuona hato SIMAMISHA fikiria ni mumeo au boyfriend wako utatafsiri vp? ... HAKIKA HAUWEZI KUMUELEWA NA WALA HUTOTAKA KUWA NAE. SASA KAMA UNAKUBALIANA NA HILI JIBU NI RAHISI SANA KWA SWALI LENU HAPO JUU.

Kumbuka siku zote MWANAUME hapendi mpaka ATAMANI kwanza. Hivo KUTAMANI kwanza alafu UPENDO unafuata.

ILA JINSI GANI NATAMANI NAKUJIKONTROO. HIYO NI MADA NYINGINE!

Naomba Kuwasilisha!

Obat Perangsang Wanita said...

I like it this really good information.

Vimax Asli Canada said...

I like it this blog information, thanks for sharing

jaya sehat said...

I like it this blog information, thanks for sharing

Obat Kuat Asli said...

I like it this blog information, thanks for sharing

poker said...

PROMO DELIMA
poker online | Agen Domino | Agen Poker|Kumpulan Poker | bandar poker | Judi Poker | bandar qiu | Judi online terpercaya

Bonus yang kami sediakan :
* TO (Turn over) sebesar 0.3% yang akan di kami bagikan setiap hari senin
* Bonus referal sebesar 10%

Ayo segera daftarkan diri anda dan bergabunglah bersama kami !!
Delimapoker.com Situs Agen Poker Online Terpercaya di Indonesia akan melayani Anda dengan profesional, memproses depo/wd dgn cepat.
Come join and be a winer with us !!

Untuk info selanjutnya silakan chat ke :
Livechat_____: delimapoker
BBM__________: 7B960959
Facebook_____: Facebook
Phone number_: +85595678845
pendaftaran___http://www.delimapoker.com/?ref=19860605

Unknown said...

Ahaha Mswati's Girl Wazuri