Friday, April 12, 2013

KUMBE WAMAKONDE WANAOGOPA KUFA...!



Inaelezwa kwamba Maziko Wamakonde huwa na maombi tofauti na yale yanayofuatwa na madhehebu mengine. Badala ya Sheikh au Kasisi kusoma dua, Wamakonde wana desturi ya kuieleza maiti maombi na maonyo ili marehemu huyo asije patwa na madhara wala asiandamwe na mikasa katika safari yake huko aendako, na pia ndugu wanaobaki nyuma wasikabiliwe na mabalaa na mikosi ya aina yoyote. Wenyewe wanaamini kwamba mabalaa huongozana, yaani likitokea moja hufuata la pili, la tatu na kadhalika. Kwa mujibu wa simulizi zao, kuna madai kwamba pale mambo hayo ya mila yanapopuuzwa vifo mfululizo hutokea katika familia husika.

Mkuu wa mazishi Huieleza maiti wakati wa maziko:

“Ndugu umeacha jembe, mshale, shoka, nyumba na kazi kwa hiyari yako mwenyewe, hakuna aliyekulazimisha kufunga safari hii, ile wewe mwenyewe umeazimia. Umetuacha sisi huku nyuma kwa hiyari yako mwenyewe, Hivi, ufikapo kwenye ukomo wa safari yako, ukaeleze yanayokuhusu wewe binafsi. Wakikuuliza  ‘Wako wanadamu wengine waliobaki?’ ukawajibu, ‘hapana.’ Ujitahidi kuwathibitishia kwamba ni wewe tu peke yako, hakuna mtu mwingine aliyebaki.”

Kwa maneno hayo, inadhihirisha wazi kabisa kwamba waliobai nyuma wanaogopa kufa. Ingawa wanajua kuwa kufa kupo, ila kama kunaweza kukwepeka basi ombi lao lisikilizwe! 

Hata hivyo inadaiwa kwamba mila hii bado inafuatwa na Wamakonde wa Msumbiji, tofauti na Wamakonde wa Tanzania ambao mila kwa kiasi kikubwa zimeathiriwa  muingiliano wa makabila na dini hizi za mapokeo

7 comments:

Vimax Asli said...

I visited several web pages however the audio quality
for audio songs existing at this website is truly fabulous.

Alat bantu sex said...

I like it this really good information.

Meizitang Botanical said...

nice blog and article, thanks for sharing

Vimax Asli Canada said...

I visited several web pages however the audio quality
for audio songs existing at this website is truly fabulous

jaya sehat said...

nice blog and article, thanks for sharing

Vimax Canada said...

thanks you for sharing

zarena cantik said...

good article, thanks you