Wednesday, April 8, 2009

NIKIKOSEA MNIVUMILIE

Hata hizi ziliwahi kukosewa

Wakati mwingine ukikuta kuna makosa ya herufi kwenye Blog hii, naomba uyavumilie, kwani hilo ni kosa la kiuchapaji tu. (Typing error)


Kama hutaki kukubali kama hilo ni kosa la kiuchapaji, basi ngoja nikwambie ni kwa nini.


Mwaka 1985 , Yugoslavia ilitoa noti mpya. Katika noti hizo kulikuwa na picha ya Rais wa zamani wa nchi hiyo, Hayati Josip Broz Tito (7 May 1892 - 4 May 1980). Lakini tarehe ya kifo chake kwenye noti hizo ilikuwa imekosewa.


Hebu niambie, noti ina maandishi gani mengi hadi ikosewe tarehe? Lakini hebu niambie inabidi watu wangapi waipitie noti hiyo kabla haijaidhinishwa kuchapwa?


Naamini ni watu wengi tu waliipitia lakini bado ilikosewa!


Naomba mnivumilie kwa mcharazo….

4 comments:

Mzee wa Changamoto said...

Duh!! Ni kweli twahitaji kuvumiliana. Lakini sasa mtu akigundua akwambie ama kukuvumilia kunamaanisha "kumezea?"
Usijali, charaza tu mama

Koero Mkundi said...

Kaka Mubelwa, kukosolewa ni muhimu, bali nimeomba kuvumiliwa tu,
Nikikosolea naamini ndio njia sahihi ya kujifunza zaidi na zaidi na hivyo kuwa bora katika eneo hili la kublog. Au sikueleweka?

Yasinta Ngonyani said...

Kukosea ni moja ya maisha, usipokosea basi huwezi kujifunza kitu!

kamala Lutatinisibwa Lutabasibwa said...

tusipokosea maanayake hatutendi lolote i.e wasiokosea ni wale wasio tenda tu!

lakini kuna makosa mengine duu

kuna bintimmoja maarufu kama Irene malonga, alisoma taarifa ya habari pale itv, badala kusema watu kumi, pale kwenye herufi 'i' ya kumi akaweka herufu 'a' na hivyo kusomeka ile kitu nisiyoweza kutaja ili nisilazimike kuomba radhi. basi taarifa ya habari ilikaa kimya dakika kadhaa na hadi sasa sikuwahi kumuona tena eti kisa? katamka a' badala ya i'

tamu hiyo