Friday, October 29, 2010

WANANCHI WENZANGU,SAFARI HII TUSIDANGANYIKE!


Unapokuta nchi ambayo wananchi wake wamekata tamaa kutokana na kutelekezwa na serikali iliyoko madarakani huku ikiacha uchumi umekumbatiwa na matajiri wachache wasio na utu, basi huna haja ya kuchanganyikiwa badala yake inabidi ujiulize unachojifunza kutoka katika nchi hiyo.

Huenda umejifunza hatari ya wananchi hao kuendelea kukishabikia chama hicho na kuendelea kukipa ridhaa ya kuwaongoza kwa kuahidiwa maisha bora na matarajio yasiyotekelezeka na yaliyoshindwa ndani ya miaka mitano iliyopita.

Lakini huenda pia umejifunza jinsi ilivyo rahisi kuwadanganya na kuwahadaa masikini kwa kuwapa vitu kama fulana, kofia na khanga ili waendelee kukupa mamlaka ya kuwaongoza hata kama huna tija kwao.

Wewe mwananchi amka, kura yako ndio zahanati yako, ndio barabara yako, ndio shule yako, ndio miundo mbinu yako na ndio itakayokuwezesha kujijengea makazi bora.

Sasa hivi tusidanganyike……..tuchukue maamuzi magumu.

Mungu ibariki Tanzania, Mungu tubariki tupate kiongozi anayejua muarobaini utakaomaliza matatizo yetu ya kiuchumi.

Ahsanteni kwa kusoma maandishi haya