Saturday, May 30, 2009

KOERO SAFARINI!!!!!

Kwa herini ya kuonana........
Kwa wanablog wenzangu na wasomaji wa blog hii ya VUKANI.

Kwa masikitiko makubwa napenda kuwafahamisha kuwa sitakuwepo mtandaoni kwa muda usiojulikana kutokana na kuwa safarini.

Ingawa ninapokwenda kuna mtandao lakini majukumua yanayonipeleka huko nadhani yatanichukulia muda mwingi, kwa hiyo ninayo matumaini hafifu ya kuonekana mtandaoni.

Kama nitapata nafasi basi naweza kupita japo siku moja moja hapa VUKANI kuwasalimia na kuwajulia hali pia nitakuwa nikiwatembelea wanablog wenzangu kama nitapata nafasi ili kupata habari, hekima na ujinga kidogo.

Nawatakia kila la heri na mungu akipenda tutaonana wakati ujaooooooo

6 comments:

Anonymous said...

Safiri salama Koero.
Huko uendako ufanikiwe katika mipango yako.
Salam kwa wanajamii wote, utukumbuke na uwasisitize wenyeji wako kuhusu matumizi mazuri ya mtandao wa intaneti.

Koero Mkundi said...

Ahsante sana dada Subi,
ukweli ni kwamba nilikumiss sana dada yangu, nakushukuru sana kwa kunitakia safari njema...
Mungu akipenda kesho asubuhi sitakuwepo DAR...
Nitakuwa Balozi mzuri wa kuzitangaza blog zetu huko niendako.....

Koero Mkundi said...
This comment has been removed by the author.
Yasinta Ngonyani said...

Koero nakutakia safari njema huko uendako. Najua Mungu atakuwa nawe na utasafiri salama. Ila binafsi nitakumiss sana. SAFARI NJEMA

mumyhery said...

safari njema koero Mungu akutangulie

Mzee wa Changamoto said...

Dada hilo tabasamu lako kwenye picha na hilo pozi lako nimelipenda. Sitakutaja maana wakati nawapiga hii picha tulikubaliana nisimwambie mtu wewe ni nani kati ya hao. LOL.
Sasa niseme nini? Kuwa ntaku-miss? Kuwa nta-miss story zako? Kuwa nta-miss chat zako? Kuwa ntaendelea kukuombea huko uendako?
Najua unajua kuwa sote tunajua kuwa iko ilivyo kwa namna ilivyo kwa kuwa sote ni ndugu.
Yote hapo juu yatatokea na nina imani tutakuwa pamoja soon.
Pamoja Daima na safari njema