Friday, February 19, 2010

LEO TUJIFUNZE NAMNA YA KUOMBA MAJI KWA LUGHA ZA MAKABILA TOFAUTI TOFAUTI

Kina mama wakitoka kuteka maji kisimani

Ndugu wasomaji wa kibaraza hiki, leo nataka tujifunze namna ya kuomba maji kupitia lugha za makabila tofauti tofauti.

Hivi karibuni nilikwenda Wilayani Babati, kule nikakutana na watu wa kabila moja liitwalo Wasandawi, nilikuwa na kiu, lakini nilipata tabu sana kuomba maji maana lugha pekee ambayo nilitakiwa kuwasiliana nao ilikuwa ni Kisandawi, basi ilikuwa kaazi kweli kweli.

Kipare:
Nighenja mazi ya kunwa=Nisaidie maji ya kunywa

Kinyawezi:
Nalilomba minze kakunwa=Naomba maji ya kunywa

Kichaga:
Ngikundi Mringa= Naomba maji ya kunywa

Kingoni:
Nitangatilai manji mlongo wangu=Naomba maji ya kunywa ndugu yangu

Kimasai:
Njaaghe Ngare= Naomba maji ya kunywa

Kihehe:
Ndisuka Ululenga= Naomba maji ya kunywa

Kimeru:
Ngitelewa Mringa= Naomba maji ya kunywa

Kijaluo:
Miaa pi= Naomba maji ya kunywa

NIMEPATA MSAADA KWA MJUVI WA LUGHA YA KIJAPANI
Kijapani:
Kwanza inabidi useme:- 1. kao nodo itai - nina kiu

2. mizu nomu itai - nina hamu ya kunwya maji

Ukisha sema moja kati ya hayo hapo juu ndio unaunganisha na lingine kati ya haya hapa:-

1. omizu kudasai

2. omizu chodai

3. omizu onegai shmasu

Kihaya:
Ninshaba amaizi= Naomba maji ya kunywa

Haya wengine mtajazia hapo.

17 comments:

Yasinta Ngonyani said...

Heee! wa msikana veve unileki hoi! Nimenukuu "Kingoni:
Nitangatilai manji mlongo wangu=Naomba maji ya kunywa ndugu yangu"

Pia unaweza ukasema nimwomba manji gakunywa.= naomba maji ya kunywa
Na halafu Kimanda Nisuka manji gakunywa= Naomba maji ya kunywa

Masangu Matondo Nzuzullima (MMN) said...

Kisukuma (Kinyantuzu) - Nalilomba minzi agung'wa au nagulombaga minzi agung'wa

Yasinta Ngonyani said...

Samahani hapo kwenye Kimanda nilikosema unajua kinafanana sana na kingoni Ni hivi Nisuka masi gakunywa. Na pia kwa kiswid ni:- Kani jag be att får ett glas vatten

o'Wambura Ng'wanambiti! said...

Kijita atasema mt simon....lol

Kisimbiti: Ndasabha amanshe ghukunywa

Koero Mkundi said...

Dada Yasinta, hicho Kiswidi, naomba utufundishe namna ya kutamka kwa kiswahili, maana mwenzako huku ulimi umeteguka

mumyhery said...

Koero, kwa jinsi ulovyo andika kijapani Watashi wa ina maana mimi
omizu maji, kwa jinsi ulivyo andika ina maana MIMI MAJI

chib said...

@ Mumyhery DUH!

Yaani ndughu dhangu wapare wao hawajui kuomba ila kuthaidiwa thu!

Love this post

Mwanasosholojia said...

Burrrrdaaani na hazina ya lugha zetu!

Anonymous said...

NIGAILE MACHI YA KUNYUWA - naomba maji ya kunywa. Ifakara hiyo ila sijui ni kimbunga, kindamba au kipogoro na kwa kizulu NG'ICELA AMANZI - naomba maji

Mbele said...

Kimatengo: "Naa masi ga kuunywa."

MARKUS MPANGALA said...

Mie simo

Mija Shija Sayi said...

Kidachi, Ik wil water om te drinken, au Kan ik heb water te drinken.

**'Wil' tamka vil, na 'Water' tamka 'Vata'

Yasinta Ngonyani said...

okey Koerounataka matamshi ya kiswid kwa kama kiswahili yaani kan jag be att får ett glas vatten utatamka hivi:- kani yogu be ati forr eti glasi vatteni.

Masangu Matondo Nzuzullima said...

Kama mwanaisimu, hapa nimefaidika sana!

Unknown said...

Dada Yasinta samahani naomba nikukosoe kidogo kwa kuwa wote tunaelimishana.
Hapa unalewa kusema:
Kan jag få ett glas vatten?

Ukitaka kutumia lugha ya upole utasema:
Skulle jag kunna få ett glas vatten?.
Nipo likizoni Dar. Napatikana kwa namba 0716 333270


Skulle jag kunna få = could I have/receive

Unknown said...

Dada Yasinta samahani naomba nikukosoe kidogo kwa kuwa wote tunaelimishana.
Hapa unalewa kusema:
Kan jag få ett glas vatten?

Ukitaka kutumia lugha ya upole utasema:
Skulle jag kunna få ett glas vatten?.
Nipo likizoni Dar. Napatikana kwa namba 0716 333270


Skulle jag kunna få = could I have/receive

gaoria said...

Tang'a amanche gakunywa (kikurya)