Saturday, March 19, 2011

UTABIRI LONGO LONGO!



Aliyoyatabili Sheikh Yahaya 25/03 /2010 Haya hapa:



Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana, Mnajimu maarufu Afrika Mashariki na Kati, Sheikh Yahaya Hussein, alisema

1......
.Rais wa Zanzibar, Amani Abeid Karume, ataongezewa muda wa kuendelea na wadhifa huo.

2.......
Mchuano wa kugombea urais wa Zanzibar utakuwa na ushindani mkubwa kuliko miaka iliyopita.

3......
.Robo tatu ya wabunge walioko madarakani wataanguka na sura mpya zitakayoongezeka zitakuwa ni za wanawake.

4......
Hakutakuwa na uchaguzi mkuu kwa mwaka huu wala mpasuko ndani ya CCM.

5.....
.Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samuel Sitta, ataendelea kushika wadhifa huo kwa kuwa nyota yake inang'aa vizuri.

6......
Viongozi wenye tuhuma kama Waziri Mkuu aliyejiuzulu, Edward Lowassa, hawatang'aa kisiasa hadi mwaka 2015.

7......
Kutatokea harusi za viongozi pamoja na vifo vya watu maarufu, matatizo ya kifedha na kiuchumi, kulipuka kwa volcano, ukame na matetemeko ya ardhi.

8.....
(CCJ) kimetabiriwa kuwa hakitaweza kukibomoa Chama Cha Mapinduzi (CCM) kutokana na kitendo cha viongozi wake wa muda kwenda kulilia kwenye kaburi la Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Nyerere, na kwamba sababu nyingine ya kukikwamisha ni jina walilolichagua.CCJ kingetumia jina la CCN.

CHANZO KILIKUWA: NIPASHE


9 comments:

Masangu Matondo Nzuzullima (MMN) said...

Ni longolongo asilimia 100% !!!

Fadhy Mtanga said...

mimi ni mmojawao wale wasiobabaishwa na utabiri wa shehe huyo wa Mwembechai.

emu-three said...

Hivi ni shekhe wa Mwembe chai, hata mimi siamini mambo hayo, na nashindwa kwanini wanamuita sheikh , wakati mamabo hayo katika imani yake hayatakiwi...lakini ndio hivyo ukimuuliza atakupa sababu kibao na hata ushahidi...wapo wengi hao, tangu enzi hizo, kwani hata akina Frauni, nk walikuwa wanatoa sababu kibao kuwa wao ni `nusu miungu'...au sio! Sasa hivi wanaingiza mambo ya siasa kuegemea kwenye dini , ...unajua kwanini , umaarufu, unajua kwanini, kutafuta `kula'
Kazi ni siku hiyo ya hukumu, kila mtu atabeba mzigo wake mwenyewe!

emu-three said...

Hivi ni shekhe wa Mwembe chai, hata mimi siamini mambo hayo, na nashindwa kwanini wanamuita sheikh , wakati mamabo hayo katika imani yake hayatakiwi...lakini ndio hivyo ukimuuliza atakupa sababu kibao na hata ushahidi...wapo wengi hao, tangu enzi hizo, kwani hata akina Frauni, nk walikuwa wanatoa sababu kibao kuwa wao ni `nusu miungu'...au sio! Sasa hivi wanaingiza mambo ya siasa kuegemea kwenye dini , ...unajua kwanini , umaarufu, unajua kwanini, kutafuta `kula'
Kazi ni siku hiyo ya hukumu, kila mtu atabeba mzigo wake mwenyewe!

kamala Lutatinisibwa Lutabasibwa said...

LOLIONDO

Upepo Mwanana said...

Kazeeka, hata na utabiri nao mtu huzeeka nao.
Nasikia kesha staafu rasmi, na sasa mtoto wake ndio msemaji

chib said...

Kuna njia nyingi za kutafuta pesa jamani. Hiyo nayo ni ajira

Anonymous said...

shekhe yahaya ni usalama wa taifa alipelewa zanzibar kikazi kwenye miaka ya70 alifukuzwa zanzibar kwa kumnajisi mtoto wa kiume mdogo huo ndiyo ulikuwa nwisho wake kukanyaga zanzibar muda huwa kulikuwa na serikali ya kulindana akataye tutaleta ushahidi hata kwa MUUGU huyu mzee ni muharibifu hana lolote iko siku MUUGU atamuathiri

John Mwaipopo said...

hivi kuna watu wanamuamini huyu mjamaa mpaka leo? hata zamani hakustahili kuaminiwa. ni mchumia tumbo nambari wani kwa akina fulani (mnawajua)

chib hapo juu amesema yote