Sunday, March 7, 2010

LEO NI SIKU YA KUZALIWA YA DADA FAITH HILARY AKA CANDY 1 WA KIBARAZA CHA MY LITTLE WORLD

Kabinti ketu Faith Hilary

Faith Hilary wa My Little World Blog

Katika viunga vya Jambiani ndani ya Visiwa vya Zanzibari, kunakopatikana zao maarufu la Karafuu ndipo historia ya binti huyu ilipoanzia.

Ikumbukwe kwamba ukanda huo wa Pwani wananchi wake bado wanaenzi tamaduni zao hadi leo hususan lile Tamasha maarufu la Mwakakogwa, tamasha ambalo naweza kulifananisha na lile tamasha maarufu kule Brazil la Samba, ambalo huwakusanya wabrazil katika viunga vya Rio De Janeiro.

Alizaliwa hapo mnamo tarehe 07/03/1991, Visiwani humo na akiwa bado ni binti mdogo wazazi wake walihamia kikazi Jijini Dar Es Salaam huku Tanzania Bara.

Binti huyu aliendelea kukua kwa umri na kimo, na alipofikisha umri wa kwenda shule, wazazi wake walimpeleka shule, akianzia na chekechea hadi alipomaliza kidato cha nne hapa hapa jijini Dar Es Salaam.

Leo hii anaposherehekea siku yake ya kuzaliwa, yuko Ughaibuni akiendelea na masomo yake ya elimu ya juu.

Ni furaha iliyoje kwa binti huyu kusherehekea siku yake hii muhimu ya kuzaliwa huku akiendelea kufukuzia ndoto yake, ambayo hata hivyo siku si nyingi zitatimia.

Pamoja na kukutakia kila la heri katika kusherehekea siku yako hii ya kuzaliwa, pia ninao ujumbe muhimu kwako:

“Dada Candy, ni jambo la kujivunia kuwa na dada mdogo mwema kama wewe. Kila jambo muhimu nililojifunza hapa duniani, kwa kiasi kikubwa lina mchangao wako, mimi na wewe naamini tutakuwa wadada wapendwa maishani, kwani kwa muda tuliofahamiana yapo mengi ya kujivunia ambayo tumejifunza. Namshukuru muumba kwa kunipa dada mdogo mwenye hekima kama wewe. Ningependa siku hii iwe ni kumbukumbu kwetu katika kudumisha undugu wetu wa hiyari”

Happy Birthday mdogo wangu Faith Hilary aka Candy1

6 comments:

Mija Shija Sayi said...

Candy1 Kumbe mdogo hivi!!!! Duh lakini kichwani mkubwa ndo maana sikuwahi kuhisi umezaliwa mwaka niliomaliza form four.

Happy birthday Mwanangu..lol!

Mungu azidi kuwa nawe daima na daima, akili zako zizidi mara dufu.
AMEN.

Yasinta Ngonyani said...

Mija nawe! ok Hongera kwa siku ya kuzaliwa Candy1 nakutakia miaka mingi na uwaone wajukuu wakopia.

Upepo Mwanana said...

Hongera Faith. Kumbe hata mimi kakubwa kidogo!!!

Faith S Hilary said...

hahahahaha da Mija, yes bado mtoto mdogo! lol...hehe asante though!

Dada Yasinta - Mungu akijaalia! Amen!

Hahaha Upepo Mwanana...now you know eh? lol thanks everyone!!

Asante sana dada Koero, I am really thankful to call you my sister! Thanks for the wishes! Love u!! xx

MARKUS MPANGALA said...

Duh! macho hunena,
kinywa chasita
umri kuusikia
mzaha au kweli sana,

CAND 1 ON TOP OF THE WORLD. duh mdogo wangu kwelikweli ha ha ha ha ha jamani maisha ya siku 60 haya bwanaaa ha ha ha ha ha ha

HERI TUMBO LILILOKUZAA Cand 1

Simon Kitururu said...

Kwa mara nyingine Happy Birthday Faith!