Thursday, August 26, 2010

MLININUKUU VIBAYA!

Sikuwa na maana hiyo, nahitaji sana kura zenu!

4 comments:

MARKUS MPANGALA said...

NANUKUU "kama TUCTA wananishinikiza niongeze mishahara kwa sababu watanipa, basi sihitaji kura zao". Shinikizo la TUCTA iliktumiwa kwa tishio la kuninyima kura, sitaki kura zao. Na wakiandamna nawatuma polisi wawasambaratishe"(MWISHO WA KUNUKUU).
>>>>>>>>>>>>>>>>>>

Ukiangalia kauli hiyo na ambayo iilitamkwa na RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Jakaya Mrisho Kikwete. mimi mcharuko namuunga mkono akiwa Rais wa nchi. Maana siwezi kuongeza mshahara wa mtu eti kwakuwa nispofanya hivyo utaninyima kura yako. Ujinga gani huu. Jakaya akiongea akiwa Rais wa nchi nimeamua sasa kumwunga mkono kwa kauli hiyo akiwa Rais wa jamhuri ya muungano na akitamka akiwa mkuu nchi. Hilo hata ningekuwa mimi mzee wa lundunyasa kataa kura hizo. Ni kwanini waseme wataninyima kura wakati madai yao hayakuhusiana na suala la kugombea urais. Wanyime tu kwani nchi hii siyo ya wafanyakazi peke yao. wasifikiri kura laki tatu tu ndizo zitamfanya awe rais. wapo watakaopiga kura na NATAMANI TUCTA WASIMCHAGUE KIKWETE HALAFU TUONE. uongozi wa TUCTA wasifikiri wanatawala akili za wafanyakazi wote. naamini kati ya kura hizo laki tatu za wafanyakazi wapo watakao mpigia kura Kikwete. Ingawa mimi siyo mshabiki wake wala mfuasi wake, lakini ningekataa kura za wafanyakazi kwa shinikizo lao la kijinga. nataka kuwaambia kitosho cha kumnyima kura kikwete ndiyo maangamizi yao. kwani hata kile walichotakiwa kukipata hawatakipata. nawaona hawana msimamo mmoja, wangesimamia hoja zao siyo kutoa kitisho cha kunyima kura, hiyo walihama katika hoja ya msingi, yaani nyongeza ya mishahara na punguzo la kodi. Vinginevyo someni hapa;

www.fananninyasa.blogspot.com, nimeandika suala moja la kihistoria kuhusu viongozi wa wafanyakazi. kifupi nimejitoa katika kuwatetea baada ya kuona wanataka kutuingiza wote kwenye mtego wao. nimeandika hivi VIONGOZI WA TUCTA KUWANIA URAIS MWAKA 2015 AU 2020?, siwaungi mkono tangu walipohamisha hoja kutoka dai la wafanyakazi hadi pilau za kura.

KWA SASA
kitu ambacho washauri wa kisiasa wa kikwete wanashindwa kumwambia ni hiki; wakati akikataa kura za wafanyakazi alikuwa Rais wa nchi. LAKINI sasa yeye ni MGOMBEA URAIS hivyo hata wakisema afafanue kauli yake haita saidia.

sisi watanzania tunataka KUDEKA SANA tunataka afafanue nini wakati mlishasikia kauli yake? Mlitegemea sasa aseme nini kama mgombea kuwa hataki kura za wafanyakazi.

TUNAHITAJI SOMA REFU sana la kueleweshana maana vyombo vya habari vinaposhupalia hilo vinachafua ukungu na habari znenye utashi kwa wananchi. TUWE MAKINIA katika kuchanganua SIASA.
kwasababu wanazuoni wa siasa walisema na kwa hili nawaunga mkono kwamba; POLITICS IS ART OF THE POSSIBLE. mlitaka mgombea kikwete aseme hataki kura hizo. tutofautishe urais na ugombea. hata kama ni yuleyule.

Maisara Wastara said...

Koero mie bado nachanganyikiwa, si alisema hazitaki kura zao? (Kura za wafanyakazi). sasa waliomnukuu vibaya ni akina nani?

emu-three said...

Siasa ni ukweli wenye uongo ndani yake, jadilini, mtagundua

Anonymous said...

Kwani alimaanisha nini aliposema hahitaji kura zao?

Au ilikuwa ni ZE COMEDY TU?